Picha rasmi ya Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania,Jakaya Mrisho Kikwete, imebadilika.Kama inavyoonekana pichani,picha ya Rais iliyoko kushoto ndio inakuwa picha rasmi mpya.Iliyopo kulia ndio iliyokuwa ikitumika mpaka hapo jana yalipotangazwa mabadiliko hayo.Haitotumika tena. Aliyezishikilia picha zote ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo, Kassim Mpenda. Hapo alikuwa akiwaonyesha picha hizo waandishi wa habari jijini Dar-es-salaam.Kwa hiyo kama ofisi yako inahitaji au ni mojawapo ya zile ambazo kiutaratibu ni lazima ziwe na picha ya Rais fanya hima uendane na mabadiliko haya.
1 Comments
jk..keep on ...